PICHA ZA WANA USCF-SJUT KATIKA TUKIO LA UZINDUZI WA ALBAMU YA CHOIR YA NEW JERUSALEMU TAREHE 5/7/2015

MGENI RASMI AKIBARIKI DVD ZA ALBAMU YA" MUNGU KWETU SISI NI KIMBILIO"(kulia)TUKIO LA UZINDUZI WA ALBAMU YA CHOIR YA NEW JERUSALEMU TAREHE 5/7/2015

SHEREHE YA KUWAAGA WAHITIMU WANAKWAYA 24 JULY, 2015.

Uongozi wa the New Jerusalem choir ya USCF-CCT St. John's University of Tanzania Tunapenda kuwashukuru wote mliojumuika pamoja nasi kuwaaga wanakwaya wahitimu walionza masomo yao mwaka 2011 na 2012,

KUTIMIA KWA UNABII WA NYAKATI ZA MWISHO

Dalili ya Mvua ni mawingu, hivyo kwa mtu mwenye busara, aliyeanika nguo zake nje anapoona tu mawingu yametanda kila mahali, anajua kwamba mvua wakati wowote inaweza kunyesha, na hakika atafanya haraka kwenda kuzianua nguo hizo.

Tunatoa Huduma ya Kutengeneza na kuendeleza Website na Blogs for free

Blog hii ya USCF-SJUT imetengenezwa na inaendelezwa na Joel Elphas kwa kushirikiana na USCF-SJUT. kwa mawasiliano kuhusiana na kuendeleza Blog hii wasiliana nae kwa namba 0757 755 228 au 0655 755 228 au elphasjoel@yahoo.com Pia tunatoa huduma za kutengeneza Website kwa bei nafuu pamoja na Blog

MAOMBI YENYE UWEZO WA KUPASUA ANGA

Moja kati ya silaha kuu, ambayo inamwezesha mtoto wa Mungu kushinda vita dhidi ya majeshi ya giza, ni maombi. Hofu kubwa kwa shetani na majeshi yake, ni pale anapokuwapo mtu mwenye nguvu ya kuzalisha maombi yaletayo moto, na hatimaye kuleta athari kubwa sana katika ufalme wa giza.

Sunday, May 29, 2016

NJINSI YA KUMUTUMIKIA MUNGU ALIYE HAI

Bwana asifiwe mwana wa Mungu,napenda tushirikiane katika neno hili(NJINSI GANI YA KUMUTUMIKIA MUNGU ALIYE HAI).

KUPITIA JUHUDI ZAKO KATIKA KUMTUMIKIA MUNGU INAWEZEKANA UMEPAMBANA NA MAZINGIRA MAGUMU KATIKA KUIFANYA KAZI YA MUNGU AMBAYO NDANI MWAKO UMEPEWA INAWEZEKANA IKAWA NI UIMBAJI,KUHUBIRI,SHUHUDA,KUTUNZA WATUMISHI WA MUNGU,KUWAJALI WASIOJIWEZA  YAANI YATIMA NA WAJANE NA KAZI ZINGINE ZA KIROHO NA ZA KIMWILI AMBAZONI HALALI KWA MUNGU WA MBINGUNI.

KATIKA KUZIFANYA KAZI ZA MUNGU NI LAZIMA UWE NA SILAHA ZIFUATAZO AMBAZO ZITAKUSAIDIA KUMUTUMIKIA MUNGU KWA UAMINIFU:
1.KUWA TAYARI WAKATI WOTE
MTUMISHI WA MUNGU TUMIKA WAKATI WOTE HAIJALISHI UKO WAKATI WA DHIKI AU WAKATI WA RAHA,MUNGU ANAPENDA WATU WANAOMWAMINI MUNGU WASIMAME KUMTUMIKIA HATA WAKATI AMBAO NI MGUMU KWAO ILI AWEZE KUJUA NI KWELI WANAMWAMINI KATIKA  KAZI ALIZOWAPA,MFANO MTUME PAULO ANASEMA KATIKA  2TIMOTHEO4:2 UWE TAYARI WAKATI UKUFAAO NA WAKATI USIOKUFAA.KUPITIA KITABU HIKI MTUMISHI SIMAMA WAKATI WOTE UFANYE KAZI YA BWANA NA MUNGU ATASHUKA KATIKA WAKATI AMBAO WEWE UNAONA HAUWEZI ILI BARAKA ZA MUNGU ZIWE NAWE SIMAMA IMARA WAKATI WOTE KATIKA YA MUNGU UNAYOIFANYA.

2.KUWA MVUMILIVU
SIMAMA KWA UVUMILIVU KATIKA KAZI YA MUNGU UNAYOIFANYA MAANA KATIKA KUVUMILIA MUNGU ATAKUBARIKI KWA KIWANGO CHA JUU SANA MFANO MWANGALIYE AYUBU ALIVYO VUMLIA MATESO MPAKA AKASHINDA HIVYO NAWE VUMILIA KWA UAMINIFU KATIKA KAZI YAKO(2TIMOTHEO4:2)

3.KUWA NA KIU YA HAKI KATIKA KAZI YA MUNGU UNAYOIFANYA.
"ISAYA55:1"MTUMISHI TAMANI KIU YAKO IFURIKWE NA MUNGU WA MAJESHI ALIYE HAI,KATIKA KILA HUDUMA UNAYOIFANYA TAMANI MUNGU AKUJAZE NA KIU YA HAKI ILI UENDELEE MBELE MAANA KIU YA HAKI ITAKUFANYA USIANGUKE  MAANA KATIKA KIU YAKO UTAMWITA MUNGU KWA UAMINIFU MNO KATIKA KAZI UNAYOIFANYA.


HIZI SIRAHA MPENDWA ZITAKUFANYA UIFANYE KAZI YA MUNGU KWA UAMINIFU NA KANISA LITAENDELEA MBELE.
               MUNGU AWABARIKI SANA KATIKA KAZI YA MUNGU UNAYOIFANYA .
                  EZRA 10:4.
  
                     "MWALIMU EMMANUEL ZAKAYO"
                                      
Share:

Friday, March 18, 2016


Share:

PICHA ZA KAMBI ZA MAOMBI



Share:

SHUKURANI NA PICHA

                                          TUNAWASHUKURU SANA KWA KUSHIRIKI
                                          KATIKA KAMBI YA MAOMBI
Share:

Wednesday, March 9, 2016

TAARIFA KWA WANA USCF SJUT

Tunakusalimu katika jina la Yesu kristo aliye hai.

1.MTUMISHI WA MUNGU KAMBI YETU YA MAOMBI ITAANZA IJUMAA SAA 2:00 USIKU HADI JUMATATU ASUBUHI(11-14/MARCH/2016)ITAFANYIKA KATIKA KANISA LA MORAVIAN IRINGA ROAD.MPENDWA TUNAKUKARIBISHA SANA KATIKA HUDUMA HII MAANA TUNAYOSABABU KUBWA MUNO KUSHIRIKI NAWE KATIKA HUDUMA HII KAMA BWANA ALIVYO TUAHIDI TUIDENDE KAZI YAKE KWA USHIRIKIANO (TAZAMA,JINSI ILIVYO VEMA NA KUPENDEZA,NDUGU WAKAE PAMOJA,KWA UMOJA.ZABURI 133:1).TUNAKUKARIBISHA SANA USIKOSE MAANA HAKUNA GHARAMA YA PESA GHARAMA YAKE NI WEWE KUFIKA NA KUSHIRIKI KATIKA HUDUMA HII.

2.WAHITIMU AMBAO HAWAJALIPIA GHARAMA YA CHETI MWISHO NI IJUMAA HII(11/3/2016) WEWE KAMA BADO JITAHIDI MAANA HAKUNA MUDA UTAKAO ONGEZWA KWA AJIRI YA JAMBO HILI HIVYO NI MUHIMU SANA KUKAMILISHA LIPA KWA KIONGOZI NDANI YA MUDA PIA MKUMBUSHE NA RAFIKI YAKO.







TUNAWATAKIA BARAKA ZA MUNGU ZIWAFUNIKE KATIKA MAJUKUMU YENU ZAIDI TUISHI KATIKA PENDO LAKE KRISTO.
                 LIKIZO NJEMA.
Share:

Tuesday, February 23, 2016

MAMBO MUHIMU YA KUFANYA KWA WANA USCF-SJUT NA WAPENDWA WANAKARIBISHWA SANA

Tunakusalimu katika Jina la Yesu kristo aliye hai,ungana na huduma ya USCF SJUT KUSHIRIKI KATIKA MAMBO YAFUATAYO ;
1.MAOMBI KWA AJIRI YA MITIHANI(UE)
Maombi haya yatafanyika kuanzia jumatano 24-26/02/2016 tutakutana chapel saa sita mchana kwa muda wa siku zilizoainishwa hivyo mtumishi ukiweza funga lakini kama hauwezi hauzuiliwi kushiriki.TAMANI SANA KUOMBA PASIPO KUKOMA MAANA ADUI HALALI HIVYO NI LAZIMA TUANGAMIZE KWA MAOMBI ROHO ZINAZO ZUIA MAFANIKIO YETU.(MATHAYO18:18)

2.PIA WATUMISHI TUJIANDAE KWA KAMBI MAALUMU YA MAOMBI BAADA YA MITIHANI YOTE KUISHA,KAMBI HII ITATUINUA KWA VIWANGO VYA JUU SANA KIROHO USITAMANI KUKOSA MAELEKEZO YATAZIDI KUTOLEWA NAMNA KAMBI IYAKAVYO ENDESHWA.

3.USCF ST.JOHN INAPENDA KUWATAKIA MAANDALIZI MEMA NA MITIHANI IJAYO KWA WANA SJUT WOTE,MUNGU AWABARIKI SANA KATIKA MASOMO YENU NA KAZI MNAZOZIFANYA KWA AJIRI YA HUDUMA YA MUMGU ALIYE HAI.





     TUNAWATAKIA BARAKA ZA MUMGU ZIWAFUNIKE KATIKA MAHITAJI YENU WAPENDWA-------USCF-PRCR KWA NIABA YA MWENYEKITI USCF-SJUT.
                       EZRA10:4
Share:

Saturday, February 20, 2016

TAARIFA KUHUSU VITAMBULISHO

Bwana Yesu asifiwe wapendwa katika bwana. Napenda kuwataarifu wote waliopiga picha za vitambulisho siku zilizopita waje wavichukue vipo tayari ofisi ya CHAPEL.Pia ambao bado hawajapiga picha mnakaribishwa ili muweze kupata vitambulisho vya uanachama wa USCF.










                                             USCF-PRCR
Share:

Tuesday, February 16, 2016

huduma ya ibada moravian iringa road 14/2/2016 kwaya na michael george mhubiri


Share:

Saturday, January 23, 2016

JIFUNZE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU ADHARI NA MATOKEO YA KUFANYA DHAMBI YA UZINZI/UASHERATI KWA MTU ALIYEOKOKA.


ADHARI NA MATOKEO YA DHAMBI YA  UZINZI/UASHERATI KWA MTU ALIYEOKOKA.

Katika Mithali 6:32 Biblia inasema “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake” na pia katika  Mithali 6:26 inasema “Maana kwa Malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani”



UZIZI/UASHERATI: Ni tendo la ndoa linalofanywa na mtu mume na mtu mke kinyume na mapenzi ya Mungu/ kabla ya wakati sahihi wa Mungu (Ndoa takatifu).



Ni watu wengi sana ambao wamerudi nyuma na kuanguka katika dhambi hii. Hadi sasa bado kuna kundi kubwa la watu waliokoka ambao bado dhambi hii ina nguvu juu yao na bado wanafanya jambo hili kinyume na mapenzi ya Mungu katika maisha yao.



Si kana kwamba Mungu anafuga dhambi kwa kutokuwadhihirisha hao watu na uovu wao, isipokuwa hataki jina lake litukanwe, kwa kuwa ikijulikana huyo mtu au hao watu wameanguka huenda  kutokana na nafasi zao kiuongozi, kihuduma kiushuhuda nk jina la Mungu litatukanwa sana na mataifa lakini pia hata na wale waliokwisha kuokoka. Kwa lugha rahisi hao watu au huyo mtu atakuwa ametoa nafasi ya jina la Mungu kutukanwa.



Kwa bahati mbaya sehemu kubwa ya watumishi wa Mungu katika makanisa yao hawaoni athari ya hili jambo katika upana wake kama Biblia inavyosema.   Inafika mahali baadhi yao wanawafariji wale walioanguka kwa kusema jipe moyo, tubu na Mungu ni wa rehema atakusamehe. Na wengine utasikia wanasema haukuanza wewe, Daudi naye yalimshinda sembuse wewe!!.



Wengine wanatumia maandiko kabisa wanasema ‘mwenye haki huanguka mara saba’ we mara moja tu wala isikusumbue sana tengeneza tu Mungu atakusamehe, na wengine wanasema mimi mwenyewe nilishindwa kwahiyo, hata wewe isikusumbue saana kazana tu uoe wa kwako au omba upate mume/mke. Ni kama vile watu wanatumia rehema/neema ya Mungu kuendelea kutenda dhambi tena kwa ujasiri.



Sikiliza, si kana kwamba napingana na neno au na mawzo ya hao watumishi wenzangu La hasha!. Nakubali kwamba Mungu husamehe dhambi na maovu  ikiwa ni pamoja na dhambi hii ya uasherati/uzinzi (Matendo ya Mitume 3:19 ‘Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana’).



LAKINI TAMBUA Mungu husamehe kwa sababu 2 kubwa sana:-

Ø  Moja hafurahii kifo cha mwenye dhambi ‘Ina thamani machoni pa Bwana mauti ya wacha Mungu wake’ Zaburi 116:15.

Ø  Na pili ni ili kukurejesha kwenye nafasi yako ili uweze kulitumikia kusudi lake.

Lakini je, unajua madhara/matokeo ya dhambi hii kwa mtu aliyeokoka anapoifanya? Hata kama Mungu akikusamehe/amekusamehe, unajua nini kimetokea/kilitokea kwako pale ulipofanya dhambi hii? Au je unaijua gharama ya kurejea kwenye nafasi yako aliyoikusudia Mungu?





Biblia inasema aziniye na mwanamke afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake? Huenda huwa unausoma tu huo msitari bila kujua uzito wa hayo maneno. Ni vizuri kwanza ukajua kwamba ndani ya nafsi ya mtu ndiko kwenye hisia, nia (utashi), akili, na maamuzi. KUBWA Zaidi kwa Mungu nafsi ndiyo ‘operating system’ kama kwenye computer, kwa maana ndiyo kiwanda kinachotoa tafsiri ya kila kitu ambacho Mungu anazungumza/sema na mwanadamu



MAMBO 3 YANAYOTOKEA MTU ALIYEOKOKA ANPOFANYA DHAMBI HII YA UASHERATI/ZINAA:-



1.   Kuharibika kwa mfumo wa mahusiano na mawasiliano kati yake na Mungu.



Katika  mfumo wa ufalme wa Ki – Mungu ni kawaida kwa mtu aliyeokoka na mwenye mahusiano mazuri na Mungu, kuona Mungu akiwasiliana/akisema naye kwa njia mbalimbali ili kumshirikisha mawazo na mipango yake ikiwa ni namna ya kumuongoza mtu huyo katika kusudi lake chini ya jua.  Hii ina maana suala la mawasiliano kati ya mtu na Mungu ni la kawaida kwa mtu mwenye mahusiano mazuri na Mungu wake.



Sasa mtu anapofanya dhambi hii, athari yake ni hii, dhambi inaharibu mfumo huu wa mahusiano kati ya mtu na Mungu. Na mahusiano kati ya mtu na Mungu yakiharibika mawasilano kati ya Mungu na mtu yanakatika/kuharibika pia. Ninaposema yanakatika ina maana si rahisi kwa Mungu kusema tena na huyo mtu au huyo mtu kusema tena na Mungu wake kwa sababu asili/mazingira hayaruhusu na hili linapelekea mafunuo/sauti ya Bwana kuwa hadimu kwako, kwa kanisa, kwa jamii, kwa kampuni na hata nchi tegemeana na nafasi yako katika ufalme wa Mungu.

2.   Kuharibika kwa mfumo wa kufanya maamuzi/kufikiri ndani yako.

Dhambi hii inaharibu mfumo wa kufanya maamuzi, shetani anapomuongoza mtu kufanya dhambi hii, lengo/interest yake ipo kwenye nafsi ya mtu huyo. Shetani akikamata nafsi ya mtu maana yake amekamata akili/nia ya mtu huyo, akikamata akili ya mtu huyo maana yake amekamata maamuzi yake pia. Na akikamata maamuzi yako amekamata matokeo ya maisha yako ya sasa na ya baadae.



Hivyo mtu huyu hataweza tena kufikiri mambo ya rohoni kama Paulo anavyoagiza kwa Warumi ile sura ya 8:5Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili, bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho”. Hivyo kufanya dhambi hii ni kuathiri mfumo wako wa kufanya maamuzi, na hii ina maana hata Mungu akileta wazo lake kwako huwezi kulipokea maana mfumo wa kuamua umeukabidhi kwa Shetani kwa njia ya zinaa/uasherati.



3.   Kuharibika kwa mfumo wa utiifu ndani yako.



Warumi 2:13 ‘Kwa sababu sio wale wasikiao sheria walio  wenye kuhesabiwa haki, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki”. Baada ya matokeo hayo 2 hapo juu hiki ndicho kinachozaliwa mwishoni. Ubaya wa dhambi hii inaharibu mifumo hii ambaayo ndiyo misingi ya mwenye haki. Fuatili maisha ya watu wengi sana walioanguka kwenye dhambi hii angalia utiifu wao mbele za Mungu ukoje. Nakuhakikishia utagundua ni ngumu sana kwao kutii maagizo ya Mungu kwao. Mtu wa aina hii hata Mungu akimpa maagizo ya kutekeleza hataweza kwa kuwa tayari mahusiano yamevunjika, mamuzi yametekwa .



JE MUNGU ANATAKA TUJIFUNZE NINI KUPITIA HILI? 



Unapokuwa na mahusiano mazuri na Mungu  hii mifumo yote mitatu/Mambo yote 3 yatafanya kazi vizuri na ndiyo kusudi la Mungu. Dhambi hii inapoingia inasababisha kuharibka kwa mifumo hii mitatu (MAHUSIANO,KUFIKIRI NA UTII). Kitu kibaya au kinacho muumiza Mungu ni kwamba hata kama akikusamehe pale utakapotubu, LAKINI itakugharimu sana kuirejesha mahali pake mifumo hii 3. Na ndio maana neno linasema afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake, kwahiyo utakua unakazi ya kurejesha NAFSI yako katika upya wake na ni garama sana sana tu. Kwasababu kila kilichomo ndani ya nafsi (HISIA, NIA, AKILI, MAAMUZI) kimeangamizwa. Ili kuirejesha mifumo hii maombi ya muda mrefu ya rehema na kutengeza mahali palipobomoka ni ya lazima.  



PENGINE unaweza kusema la muhimu Mungu amenisamehe, hayo mengine sijali sana. Unaweza kusema hayo maneno kama hujui/ huelewi muda unathamani kiasi gani kwa Mungu, na pia mahusiano kati ya muda na Mungu.



NGOJA NIKUAMBIE SIRI YA MUNGU NA MUDA JAPO KIDOGO; Muda na Mungu ni marafiki, na tena wote wana mahusiano mzuri sana.  Muda anaongoza maamuzi ya Mungu na Mungu anaongoza matumizi ya muda kwa kuiweka mipango ndani ya mtu na kumwagiza atekeleze ndani ya muda. Hivyo kwa Mungu muda ni muhimu sana.



Kitu gani namaanisha hapa; Mungu hakutenga/kuweka muda wa mtu kurejesha mifumo hii kwa sababu umeanguka katika dhambi. Katika kipindi ambacho wewe unatubu na kutengeneza kwa Mungu wako ili kurejesha mifumo hii, basi uwe na uhakika upande wa pili umesha athiri kusudi la Mungu duniani kupitia wewe ambalo limefungwa katika muda. Sasa kama utatumia siku tano, mwezi mmoja, miezi sita, mwaka mzima nk, kurejesha hii mifumo basi kwa kipindi hicho chote utakuwa umekwamisha kusudi la Mungu kupitia wewe. Na ndio maana Biblia inasema Shetani anawinda nafsi yako iliyo ya thamani, maana anajua akikamata nafsi yako amekamata akili, nia, hisia na maamuzi yako na hivyo amefanikiwa kuharibu hiyo mifumo na kusababisha mipango ya Mungu isifanyike kwa muda aliokusudia kupitia wewe.



Kwa Mfano; Fikiria umepangiwa na Mungu kusafiri umbali wa kilomita 500 ndani ya masaa saba (7).  Mungu amekupa gari ambalo ni kusudi lake  kwako. Hivyo litazame gari ulilopewa kama kusudi la Mungu kwako na wewe ni dereva. Sasa wewe ukaamua kuliendesha  gari bila kuweka maji kwenye injini. Baada ya kusafiri umbali wa kilomita 300 injini ya gari ikafa kwa kukosa maji na mbele yako zimebaki kilomita 200. Je unajua utakuwa umeathiri kwa kiwango gani kusudi la Mungu? Kutokana na mfano huu, unapotenda dhambi hii  je unajua ni kwa kiwango gani utakuwa umeathiri mipango ya Mungu kupitia wewe duniani kwa kipindi chote ambacho utakuwa unairejesha mifumo iliyopo ndani ya nafsi yako mahali pake?.



Kinacho muumiza/huzunisha Mungu kimsingi si kwa sababu umeanguka dhambini, lakini ni kwa sababu kuanguka kwako dhambini kunamzuia yeye kukutumia wewe mpaka hiyo mifumo yote irejee mahali pake. Hii ina maana interest ya Mungu ipo kwenye muda. Maana anajua itakugharimu wewe muda wa kutengeneza na itamgharimu yeye muda wa kukusubiri wewe utenegeze mifumo hii.



Mpendwa kumbuka hili usije sahau, Mungu hategemei wewe uanguke katika dhambi hii, maana kadri unavyoanguka ndivyo unavyokwamisha na kuchelewesha kazi ya Mungu duniani kupittia wewe. Je unajua hasara na matokeo ya kukwamisha na kuchelewesha kazi ya Mungu?



Je katika nafasi ambayo Mungu amekupa Kazini, huduma, au kanisa unachunga kwa kiasi gani nafsi yako isiharibiwe na dhambi hii? Neno linasema Matendo ya Mitume 20:28Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe”.

Naamini ujumbe huu utakusaidia kuhakiksha unafanya maamuzi ya kutofanya tena dhambi hii si kwa sababu imeandikwa tu usizini bali ni kwa sababu unampenda Mungu na unataka kuhakikisha kusudi la Mungu linafanikiwa bila kukwamishwa kwa dhambi hii.



                                                   Mwisho.

                            ******** MUNGU ATUSAIDIE. *********


Share:

Friday, January 22, 2016

FAHAMU KUHUSU SAUTI YA MUNGU KWAKO.


FAHAMU NAMNA YA KUSIKIA NA KUIELEWA SAUTI YA MUNGU ILI IKUSAIDE KATIKA KUFANYA MAAMUZI.



Lengo kuu la somo hili ni kumsaidia Mwanadamu yeyote yule aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu kujua namna anavyoweza kusikia Sauti ya Mungu na Kuielewa Sauti ya Mungu. Kwanini? Kwasababu ni wachache sana wanao sikia na kuilewa sauti ya Mungu pamoja na kuwa Mungu huzungumza nao mara kwa mara. Wengine hujiuliza swali hili; Je ni kweli Mungu anazungumza na mwanadamu hata sasa? Hili ni moja ya swali ambalo watu wengi wamekuwa wakijiuliza na kukosa majibu muafaka kwani baadhi yao hawaamini kwamba ni kawaida ya Mungu kuzungumza na wanadamu. Kama ilivyokuwa katika agano la kale, agano jipya, naam hata sasa, Mungu ni yeye yule jana na leo na hata milele.

Maandiko yanadhibitisha wazi kuwa ni kweli Mungu anazungumza na mwanadamu hata hivi leo na si Mitume na Manabii tu tunaowasoma katika Biblia, lakini hata mimi na wewe katika ukawaida wetu Mungu husema nasi.



Mungu anasema “Enyi watu, nawaita ninyi; Na sauti yangu ni kwa wanadamu” (Mithali 8:4). Hivyo ni kusudio la somo hili kuongeza ufahamu wako ili uweze kujua ni kwa namna gani Mungu huzungumza na mwanadamu na kisha nini ufanye ili kumuelewa Mungu anapozungumza na wewe. Ni muhimu kwanza tujiulize swali hili muhimu tunapotafakari somo hili, Kwa nini Mungu azungumze/aseme na mwanadamu? Jibu la swali hili, linalenga kutaka kujua sababu za Mungu kuzungumza na mwanadamu au mwanadamu anahitaji kuisikia sauti ya Mungu ili:-

       I.            Aishi sawasawa na kusudi au mapenzi ya Mungu awapo hapa duniani. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama. (Zaburi 32:8)

   II.            kujenga na kudumisha mahusiano/mawasiliano mazuri kati yake na Mungu. Kutoka 33:11 Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani

III.            kuona kama Mungu aonavyo na hivyo kutafsiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Yeremia 1:11-12 “Tena neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi. Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.



MAMBO MHUMU YA KUJUA KUHUSU SAUTI YA MUNGU

Yafuatayo ni baadhi ya mambo muhimu ya kukusaidia kuijua, kuisikia na kuielewa sauti ya Mungu, nawe hunabudi kuyafahamu na kuyatenda:-

1.     Jenga na kudumisha mahusiano mazuri na Roho Mtakatifu – Ni vizuri ukafahamu kwamba Roho Mtakatifu yupo duniani sasa akiliongoza kanisa katika kuyatenda mapenzi ya Mungu. Hivyo uwepo wa mahusiano mazuri kati yako na Roho Mtakatifu ndio ufunguo wa mawasilaino mazuri kati yako na Mungu. Biblia inasema wazi kabisa katika 1Wakorinto 2:10

Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu… vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu”. Andiko hili linatuonyesha umuhimu na nafasi ya Roho Mtakatifu katika kutusaidia kuisikia sauti ya Mungu. Hivyo jenga na kudumisha uhusiano wako na yeye, itakusaidia sana katika kiujua na kuisikia sauti ya Mungu.



2.     Ongeza ufahamu wa viashiria (signal) vya mawasiliano kati yako na Mungu Ufahamu wa viashiria (signal) za mawasiliano kati yako na Mungu ni wa lazima ili kusikia na kuielewa sauti ya Mungu. Zipo alama mbalimbali kwa kila mwamini ambazo Mungu hutumia katika kusema naye. Biblia katika 1Samweli 3:9 inasema “… Enenda, kalale, itakauwa AKIKUITA, utasema, Nena, BWANA; kwa kuwa mtumishi wako anasikia…” Kwahiyo kiashiria kimojawapo ambacho Mungu anakitumia kusema na Mwanadamu ni KUITA, naam anaweza kukuita kwa sauti itokayo kinywani pake au KWA NJIA KUKULETEA ALAMA/VIASHIRIA VYENYE KUKUFANYA UJUE MUNGU ANANIITA.



Kama ilivyo kwa jinsi ya kibinadamu anayekuita si lazima aongee, anaweza kutumia alama za mikono au hata maandishi nk, kukuita. Katika kukuita kwa njia ya viashiria/alama Mungu anaweza kuleta nguvu/msisimuko/ubaridi/maumivu fulani kwenye sehemu ya mwili wako au huzuni moyoni mwako kama ishara/kiashiria cha uwepo wake juu yako na hivyo KUTAFUTA/KUTAKA USIKIVU WAKO ILI ASEME NAWE. Hivyo ni lazima uwe na ufahamu na utafute kujua kuhusu alama/namna ya kwako ambayo Mungu hutumia kutafuta usikivu wako.



N: B Tambua kuwa Ipo namna ya kwako ambayo Mungu hupenda kusema na wewe ambayo inaweza kabisa ikawa tofauti na anavyosema na rafiki yako, Mke, Mume au ndugu yako. Ni jukumu lako kujua viashiria hivyo kwa upande wako kwa kumuuliza Roho Mtakatifu pekee ambae hutufunulia siri za Mungu. Usijefanya vitu kwa Mkumbo au kuiga kutoka kwa rafiki yako na ikakugharimu.



3.     Ni lazima ujue kutofautisha sauti ya Mungu na sauti nyingine. Hapa ndipo penye mtihani mkubwa sana kwa watu wengi mno, kama ilivyokua kwangu kabla sijajifunza kuhusu jambo hili. Ni muhimu sana kwako kulielewa ili usije ukaipuuza sauti ya Mungu kwa kudhani ni mawazo yako au ni ya Shetani au usije ukatekeleza jambo ukiamini kwamba Mungu amesema nawe kumbe Shetani ndiye alisema nawe. Shida ya namna hii aliipata Samweli wakati huo akiwa mtoto na Mungu alikusudia kumuita kwaajili ya Taifa la Israeli. Mungu alimuita kwa sauti yake lakini hakuitambua, badala yake alifananisha na sauti ya Babu yake Mzee Eli. Maandiko yanasema “Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu; basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa. Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena. Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena. Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto. Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake. Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia (1Samweli 3:2-10). Ni muhimu ukaelewa kwamba Mungu anaweza kusema na wewe hata kama uko katikati ya mkutano wa watu wenye kelele nyingi sana. Hii ni kwa sababu Mungu hatumii mdomo kusema nasi bali anatumia moyo wako kuzungumza. Moyo ndio kiungo muhimu cha mawasiliano kati ya mtu na Mungu.



Ukisoma katika Matendo ya Mitume 12:22 Biblia inasema “Watu wakapiga kelele, wakasema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya Mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho”. Kauli hii ya watu ilikuja baada ya Mfalme Herode kuhutubia watu na kutoa maneno makuu. Watu waliamini kwamba ile ilikuwa sauti ya Mungu, kumbe sivyo na matokeo yake Herode alipigwa na Mungu akafa.



Katika hili nataka nikupe Tahadhari ndugu mpendwa, kuna wakati mtu/watu au watumishi wanaweza kunena mambo makubwa na watu wakadhani Mungu wa kweli anasema ndani yao, kumbe ni mungu wa dunia hii. Na ndio maana ni muhimu sana wewe binafsi uongeze ufahamu wako katika kuijua, kuisikia na kuielewa sauti ya Mungu, ili hata mwanadamu akinena unajua kwamba hili limetoka kwa Mungu wa kweli au vinginevyo.



Naam! mpendwa zipo sauti mbalimbali ambazo zote zinalenga kupambana/kuharibu kusudi la Mungu ndani ya mtu, zipo sauti za wanadamu (wazazi, walezi, mwenza wa ndoa, viongozi wa kiroho), ipo sauti ya Shetani kupitia majeshi ya pepo wabaya nk. Ni lazima mwanadamu amjue sana Mungu kiasi cha kutosha ili kuweza kutofautisha sauti hizi. Njia au namna pekee ya kutofautisha sauti hizi na ile ya Mungu ni kuwa na uelewa au ufahamu mkubwa wa Neno la Mungu pekee, kwasababu Mungu hawezi hata siku moja kukuagiza jambo lililo kinyume na Neno lake.



FAHAMU VIKWAZO VINAVYOWEZA KUPELEKEA KUTOKUSIKIA SAUTI YA MUNGU.

Biblia imeainisha vikwazo kadhaa vyenye kupelekea mtu kutokuisika sauti ya Mungu. Nitakuonyesha vikwazo 2 vikubwa na nikupe changamoto ya kuingia ndani Kiimandiko ili kujua vikwazo vyengine:-

       I.            Dhambi au kuishi maisha ya dhambi. Mungu hapendezwi na Mtu anayeishi katika mazingira au maisha ya dhambi, (1Yohana 3:4) “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi”. Maana yake ni kuwa atendaye dhambi anakua amemuasi Mungu, kwahiyo amekwenda kinyume na sheria iliyowekwa na Mungu. Matokeo yake mtu huyo na Mungu wanakua mbali kila mmoja akiacha kujishughulisha na mwenzie. Isaya 59: 1-2 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”. Angalia lilee neno ‘HATA HATAKI KUSIKIA’.



    II.            Kukosa uaminifu. (Hesabu 12:7-8,). Mungu hupendezwa sana na Mtu aliye mwaminifu kwake siku zote za maisha yake. Kwa mtu huyo Mungu hujenga mahusiano ya karibu kwa haraka mno na hata kusemezana nae Zaidi. Maandiko yanalidhibitisha hili pale Mungu aliposema mwenyewe akiwaambia Haruni na Miriamu Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili. Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa? (Hesabu 12:5- 8). Uhusiano wa karibu sana aliokua nao Musa na Mungu ulitokana na UAMINIFU aliokua nao Musa mbele za Mungu. Mungu alimpenda na kuamua kuingilia kati kwa yeyote yule aliyejaribu kufuatilia au kugusa maisha ya Musa, hakika ni kama alikua akigusa maisha ya Mungu kwasababu haukunyamaza hata kidogo. Cheki kilichomtokea Miriamu baada ya kumsemasema Musa kwa habari ya Mke wake “Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake. Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma. Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi. (Hesabu 12:9-10). Kwa muda wako unaweza soma habari za Samweli katika ile 1Samweli 2:26-35 utajifunza kitu kuhusu uaminifu kupitia wito wa Samweli.

Ipo mifano ya wanamapinduzi wengi amabo walifanya mambo makubwa wakiongozwa na sauti ya Mungu katika kila jambo; akina Daniel, Paulo, Samweli, Yoshua na wengine wengi. Maisha ya uaminifu mbele za Mungu ndiyo ilikua silaha kubwa ya mafanikio na ushindi wao dhidi ya wengine.



MAMBO YATAKAYOWEZA KUKUSAIDIA KUJUA NA KUISIKIA SAUTI YA MUNGU KATIKA MAISHA YAKO.



       I.            Unahitaji kufahamu umuhimu wa Mungu kuzungumza/kusema nawe. Zipo sababu nyingi za Mungu kuzungumza na wanadamu laikini kubwa yenye kuzibeba zote ni ile iliyoandikwa katika Zaburi 32:8 kwamba Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama”. Kwanini? Kwasababu mwanadamu haishi duniani kwa muda ambao Mungu amemuweka kwa kusudi lake mwenyewe, bali ni kwa kusudi la Mungu pekee.

Ndivyo maandiko yanavyotueleza ukisoma kitabu cha (Warumi 8:28)Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Kwahiyo ili uweze kulitumikia vizuri kusudi la Mungu katika maisha yako sharti ni kwamba; lazima uongozwe nay eye katika njia sahihi. Na njia mojawapo ni ya Mungu kusema na wewe. Lengo lake katika kusema na wewe ni kukuongoza katika njia sahihi kwa kukuondoa kwenye makusudi ambayo yapo nje na mapenzi yake kwenye maisha yako maana imeandikwa “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani; Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi; Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni, Na uhai wake usiangamie kwa upanga” (Ayubu 33:14-18)



    II.       Ongeza ufahamu wako kuhusu ulimwengu wa roho. Mambo yote yanayotokea katika ulimwengu wa mwili yameanzia katika uilimwengu wa roho, naam maamuzi ya kile ambacho hutokea katika ulimwengu wa mwili hufanyika katika ulimwengu wa roho. Zaidi hata mapambano (vita vya kiroho) yote aliyoanayo mwanadamu katika kulitumikia kusudi la Mungu hufanyika katika ulimwengu wa roho.

Hivyo kuwa na ufahamu wa ulimwengu wa roho hususani namna ya kuishi na kuwasiliana katika ulimwengu huo ni muhimu sana kwa mwamini mwenye kutafuta kujua na kuisikia sauti/mawazo ya Mungu katika maisha yake. Kwa kuwa Mungu ni roho kama alivyo na Shetani pia. Hebu tusome habari ya Elisha na Mtumishi wake, 2 Wafalme 6:8-17. Maandiko yanatueleza kwamba Shetani nae ni roho ukisoma Waefeso 6:10-12.



Ndugu mpendwa usiruhusu yale unayoyapitia au yale ambayo watu /mazingira yanasema juu yako yabadilishe au kuongoza maisha yako, bali tafuta kuijua na kuielewa sauti ya Mungu kwenye maisha yako. Na ndiyo maana somo hili limekuja ili kukusaidia kufika mahala ambapo utaweza kuyatenda mapenzi kamili ya Mungu kwenye maisha yako.






Share:

Tuesday, January 12, 2016

wahi ibada

Mpendwa zingatia muda wa ibada zetu na Mungu atakubariki sana.
Share:

Friday, January 8, 2016

KARIBU NA SHIRIKI IBADA YA USCF-CCT KILA JUMAPILI..

Tunazidi kukumbusha na kukujulisha kwamba, ibada zetu za kila jumapili zinaendelea kama kawaida. Kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 3:00 asubuhi. Karibuni sana.
Share:

MY LUNCH IS YOUR HAPPINESS!!


Share:

Monday, January 4, 2016

Tunakusalimu katika Jina la Yesu Kristo. Uongozi wa USCF Tunawatakia Heri ya Mwaka mpya 2016. Tunakutakia Baraka za Mungu. Amen
Share:

TAFAKARI UJUMBE WA MWAKA MPYA 2016


JE UMEJIANDAAJE KUKABILI MWAKA 2016?

Nakusalimu katika Jina la Yesu Kristo. Heri ya Mwaka mpya 2016!

Ni kawaida kwa watu wengi kila ifikapo mwanzo mwa mwaka mpya kufanya maandalizi mbalimbali eidha binafsi, familia, ukoo, taasisi na hata nchi. Wengine huanza maandalizi mwishoni mwa mwaka uliokwisha na wengine hufanya mwanzoni mwa mwaka mpya. Ni jambo jema kufanya maandalizi ya kukabili mwaka kwani hukuandaa kuishi sawasawa na ulivyokusudia.

Lakini Je kama Mkristo umejiandaaje kukabili mwaka 2016? Biblia inasemaje kuhusu majira, nyakati na mwaka aliotupa Bwana?

Biblia inatuambia katika kitabu cha Mhubiri 3:1-8  kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu; Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia; Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.



Katika mistari hiyo tunaona Biblia ikielezea vitu vingi ambavyo Mungu ameviumba na kuviweka chini ya mbingu LAKINI vyote vimewekwa katika WAKATI (TIME) yake ndani ya kusudi maalumu la Mungu. Maana yake ni kwamba kila kitu ambacho Mungu amekiweka chini ya mbingu kipo/kimefungwa ndani ya muda/wakati wake maalumu na haiwezekani kukatokea muingiliano, kwani wakati ndio UFUNGUO au ndio unao amuru kitu gani kiwepo au kisiwepo. Huu ndio utaratibu wa Mungu aliouweka.



Kwanini Mungu ameweka utaratibu huo? Ipo siri ya Mungu na muda, Muda na Mungu ni marafiki tena wana mahusiano mazuri sana. Muda anaongoza maamuzi ya Mungu na Mungu anaongoza matumizi ya muda kwa kuiweka mipango yake ndani ya mtu au kuachilia majira Fulani katika mwaka na kumwagiza mwanadamu atekeleze hiyo mipango/majira ndani muda sahihi aliokusudia.



 Kwahiyo hata katika mwaka 2016, ipo mipango na yapo majira, na nyakati Mungu aliyoamuru Kuwepo na vyote hivyo vimefungwa katika muda ili viweze kutimia sawasawa na mpango wa Mungu, na Mwanadamu ndiyo amepewa hiyo mamlaka ya kufahamu na kuyatimiza yote lakini ndani ya wakati wa Mungu pekee. KWAHIYO Mwanadamu kamwe hana wakati wakwake peke yake bali kila jambo ndani ya wakati (Time) pamoja na Mungu aliye hai. Ms. 11 Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao…’



Unaweza jiuliza KUSUDI la Mungu hapa ni nini? Ukiendelea Ms. 14 utapata jibu ‘Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye’. Mungu ameyafanya hayo yote ili tu Mwanadamu amche yeye pekee na si vinginevyo.



Je tunawezaje kuyafahamu majira na nyakati Mungu alizoamuru kwa Mwaka 2016 ili tuweze kuishi sawa sawa na Mungu anavyotaka? Kama anayosema katika neno lake Zaburi 32:8Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama’.



Ukisoma 1 Wakorinto 2:9 -10 ‘Lakini, kama ilivyoandikwa, mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchungza yote, hata mafumbo ya Mungu’. Kwahiyo njia peke ni kumuliza Roho wa Mungu peke yake ndiye aliye na uwezo wa kutufunulia yote ili tuweze kujua.



Maelezo ya Mtume Paulo yanatufanya tujue kwamba katika mwaka 2016 kuna mambo mazuri ambayo Mungu amewandalia watoto wake na kwa njia ya Roho Mtakatifu tunao uwezo wa kutambua nini kinakuja kwenye kila eneo la maisha yetu hata kabla hatujauingia mwaka husika.



Tambua kwamba katika mwaka 2016 kila ufalme yaani ufalme wa Mungu (Nuru) na ule wa Shetani (Giza) kuna mambo umeyaandaa/kusudia kwa ajili yako kifamilia, ndoa, kazi, huduma, masomo, biashara, kanisa lako, taifa lako n.k. LAKINI Ni dhahiri kwamba Mungu amekusudia mema kwa ajili yako kama Neno lake linavyosema katika Yeremia 29:11a Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho’. Shetani kama ilivyo asili yake amekusudia mabaya juu yako.



Je, unakumbuka matukio ya mwaka 2015 kwako binafsi, kifamilia, kikanisa, Kitaifa na dunia kwa ujumla?   Je, unajua katika ulimwengu wa roho matukio hayo yameacha au kuzaa kitu gani? Naam chukua muda yatafakari kibiblia na kisha jiulize laiti ungejua kabla hujaingia mwaka 2015, kwamba hayo yaliyotokea yatatokea ungechukua hatua gani? 

Kumbuka lolote unaloliona katika ulimwengu wa mwili linatokea ujue, lilishatokea kwenye ulimwengu wa roho kwanza. Naam kwenye ulimwengu wa roho, ndipo una fursa ya kuona mambo yanayoenda kutokea duniani, kabla hayajatokea. Ni katika ulimwengu wa roho ndipo unaweza:-

(I)           kupambana ili kuhaikisha jambo jema ambalo Mungu amekusudia linatimia. Pia,

(II)         kuzuia lolote baya ambalo Shetani amekusudia juu yako, famila n.k katika ulimwengu huu wa mwili lisitokee. 

Kutokana na umuhimu wa kuwa na ufahamu wa nini kinakuja siku za usoni yaani mwaka 2016, imenilazimu kuandaa ujumbe huu ili ukusaidie kujua angalau kwa sehemu 2016 ni mwaka wa namna gani na ndani yake kuna nini? Hii itakusaidia sana kujua ufanye nini ili kufanya maandalizi mazuri tushirikiana na kuyakabili yale yanayokuja. 

Kila mwaka, ndani yake kuna mambo ambayo ni LAZIMA yafanyike au yatime kulingana na nyakati ambazo zimeamriwa juu yako na Taifa pia (Rejea Mhubiri 3:1). Kwa mwaka 2016 yafuatayo ni baadhi ya mambo muhimu ambayo ambayo Roho wa Mungu amenifunulia tujue Mungu alivyokusudia kwa ajili yetu watoto wake:-



1.   Ni mwaka wa kuwekeza na kukusanya (kuweka akiba) Zaidi kwa kuwa kuna mabadiliko ya kiuchumi yanakuja.

Biblia katika kitabu cha Mwanzo 41:35-36 inasema ‘Na wakusanye chakula chote cha miaka hii myema ijayo, wakaweke akiba ya nafaka mikononi mwa Farao wakakilinde kuwa chakula katika miji. Na hicho chakula kitakuwa akiba ya nchi kwa ajili ya miaka hiyo saba ya njaa, itakayokuwa katika nchi ya Misri, nchi isiharibike kwa njaa’. Maelezo haya ya Yusufu ni matokeo ya fasili ya ndoto ya Farao kiongozi wa Misri.  Baada ya kupata tafsiri yake ilibidi Taifa la Misri watumie miaka saba ya mwanzo kukusanya chakula kwa ajili ya miaka mingine saba ya njaa iliyokuwa inakuja mbele yao.

Usiogope, binafsi, sikuelezi kwamba pia katika Taifa letu kuna miaka saba ya njaa inakuja La hasha!. Hata hivyo jambo ambalo nina uhakika linaenda kutokea ni mabadiliko muhimu ya kiuchumi si tu wa nchi yetu bali Dunia nzima kuanzia mwaka 2016 ambayo yataleta athari si tu kwa uchumi wa Taifa bali mpaka mtu mmoja mmoja. Mabadiliko hayo kama yatakukuta haujajipanga vizuri kwa kuwekeza katika sekta na nyanja mbalimbali za kiuchumi itakugharimu sana. Naam! mabadiliko haya yaliyoanza kwa sehemu mwaka 2015 na kuendele kwa kasi mwaka 2016 yatakuwa mazuri kwa wale waliojiandaa kuyakabili, na si vinginevyo (asomaye na afahamu).

Hivyo nakushauri mpedwa katika mwaka 2016 fanya kila jitihada kuwekeza fedha, muda na nguvu katika kuimarisha biashara zako, kazi zako, mifugo na zaidi kuongeza vyanzo vingine vya mapato. Naam tia bidii sana katika kila utakalofanya kwa mwaka 2016 ukimtanguliza Mungu. Katika Kumbukumbu la Torati 8:18 imeandikwa ‘Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, mana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake hata hivi leo’. Hivyo tarajia kupata mawazo mapya na yaliyo bora zaidi yatakayokusaidia kupata utajiri katika mwaka 2016 kutoka kwa BWANA Yesu, naam tegemea akili zako kutakaswa na hivyo kuwa na mawazo ya ubunifu na ufumbuzi zaidi katika mwaka 2016 yatakayopelekea kukubalika na kuinuliwa kwako zaidi kushinda wengine kazini kwako.

Kama una mradi wako yaani duka au biashara yoyote usiridhike nayo ipanue zaidi au kuongeza nyingine mpya, naam chukua hata mkopo upanue wigo wako ni muhimu sana kwa kule tunakokwenda.  Sambamba na hayo anza sasa kuweka akiba ya fedha (endapo hufanyi hivyo) ambayo ni muhimu sana kwa huko tunakokwenda, ni muhimu sana ukaweka akiba yako kwenye mifuko mbalimbali ya kutunza akiba ya kijamii au ukawa na akaunti maalum kwa ajili ya akiba.

N: B KUMBUKA Tunza na zingatia sana Muda katika kila jambo, usipoteze muda kwenye mambo yasiyo ya msingi kama kuangalia Tv, Sinema masaa 24. Tunza muda na tumia vizuri muda wako, muda ni mali kwani muda ukipita hauridi tena na mafanikio yako yote yamefungwa katika Muda kama Biblia inavyosema. Kufanikiwa au kutokufanikiwa kwako kunategemea kwa kiasi gani umetumia muda wako vizuri.

2.   Ni mwaka wa kucheka kwa kuwa BWANA anaenda kuwafurahisha watu wake wale wanaomtegemea.

Ayubu 42:10 ‘Kisha BWANA akageuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; BWANA naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza’.  Ukisoma kitabu cha Ayubu sura 1-2 utaona habari za Ayubu na jinsi Shetani alivyoharibu maisha yake kwa ujumla. Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Ayubu, hata hivyo hizo ndio nyakati zilizokuwa zimeruhusiwa juu yake. Maandiko yanaonyesha kuwa baada ya Ayubu kusimama vizuri na Mungu wake katika kipindi hicho kigumu, BWANA alimrejeshea Ayubu maradufu kila kilichokuwa kimeharibiwa na Shetani yaani furaha, afya, watoto na mali zake zote. 

Vivyo hivyo katika mwaka 2016 BWANA amekusudia kutimiza ahadi nyingi kwa watu wake wanaomtegema, kile kilichoharibiwa kitarejeshwa, haki zilizopotea zinaenda kurejeshwa, BWANA anaenda kurejesha uzima katika mwili wako nk. Kama ni familia yako, ndoa yako, huduma yako, kazi yako nk Shetani aliharibu na kuteka, uwe na uhakika BWANA Yesu anaenda kuponya na kurejesha uhai tena.

3.   Ni mwaka wa amani utakaokupa fursa ya kujijenga na kutimiza mapenzi ya Mungu kwa mwaka husika

1 Waflme 5: 3-5, Umemjua Daudi baba yangu jinsi asivyoweza kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wake, kwa sababu ya vita vilivyomzunguka pande zote, hata Bwana alipowatia watu chini ya nyayo zake. Ila leo Bwana, Mungu wangu, amenipa amani kila upande; hakuna adui, wala tukio baya. Nami, tazama, nakusudia kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia Daudi baba yangu, akisema, Mwana wako, nitakayemweka katika kiti chake cha enzi mahali pako, ndiye atakayeijenga nyumba kwa jina langu’.

Maneno haya yalisemwa na Sulemani baada ya kutawazwa kuwa mfalme kufuatia kifo cha baba yake Daudi. Ukisoma Biblia yako vema utagundua kwamba utawala wa Daudi ulikuwa na vita sana, na kwa sababu ya vita na damu nyingi iliyomwagika katika kipindi chake BWANA alimzuia Daudi asimjengee Hakalu. Hekalu lilijengwa kipindi cha mwanawe Sulemani.  Naam ili Sulemani aweze kujenga hekalu vema, BWANA akampa amani pande zote na kazuia baya lolote lisitokee.

Vivyo hivyo Mungu anaenda kuleta amani juu yako kila upande katika mwaka 2016 ili utumie fursa si kujijenga wewe binafsi bali kuujenga ufalme wake kwa mwaka husika kwa kutimiza yale anayotaka kufanya juu ya Taifa, Kanisa, familia, ndoa kupitia wewe. Hii haina maana kwamba Shetani hajapanga mabaya, tunafahamu kwamba yeye ni baba wa uongo, lengo lake kubwa ni kuiba, kuchinja na kuharibu.

Amini kwamba kabla Shetani hajatekeleza mipango yake BWANA ataizuia na kupigana kwa ajili yako ili kutoathiri kusudi lake kupitia wewe kama alivyofanya  siku za Mfalme Yehoshafati, aliposema “Hamtahitaji kupigana vita, jipangeni, simameni, mkauone wokovu wa BWANA ulio pamoja nanyi, enyi Yuda na Yerusalemu; msiogope wala msifadhaike; kesho tokeni juu yao, kwakua BWANA yu pamoja nanyi” (2Nyakati 20:125), naam hivi ndivyo BWANA anavyoenda kuwashindia watoto wake katika mwaka huu.

Hakika huu ni mwaka wako wa kujijenga kiuchumi, kibiashara, kifamilia, kikazi, kwa kilimo nk. Ndio BWANA anaenda kuruhusu majira mazuri juu ya nchi yetu na kuzuia kila uharibifu uliokusudiwa juu yetu. 

Kwa uchache na kadri Mungu alivyonifunulia siri hizi kwa habari ya mambo yanayokuja siku za usoni katika mwaka huu. Hayo ni mawazo ya Mungu kuhusu watu wake na kanisa kwa ujumla kwa mwaka 2016, na daima mawazo ya Mungu ni mawazo ya amani (Yeremia 29:11), haya ambayo amesema nawe kuhusu 2016 unapaswa kuhakikisha unayafuatilia mpaka yatimie juu yako na Taifa letu pia. Namna mojawapo ya kuhakikisha haya yanatimia ni kujiwekea malengo ambayo yatatoa fursa kwa imani yako kuwa na mahali pa rejea kadri unavyozidi kuukabili mwaka 2016. 

TAMBAUA; Biblia katika kitabu cha Waebrania 12:1 inasema ‘Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana’. Ni muhimu sana ukajiwekea utaratibu wa kuwa na malengo ili yakusaidie kujua hatua zilizoko mbele yako ambazo unapaswa kuzifikia. Naam si suala tu la kuweka malengo bali kuyaweka kwa kuzingatia kile kinachokuja katika mwaka 2016. Natambua liko kundi kubwa la watu ambao wanaweza kuwa walishaweka malengo yao hata hivyo bado una fursa ya kuyaboresha (adjust) kwa kuzingatia hiki ambacho umejifunza katika ujumbe huu.

Malengo yako yatakusaidia kujua hatua unazopiga endapo zinakufikisha kule ambako Mungu anataka ufike katika mwaka 2016.

Maandiko yanasema katika Isaya 60: 1 ‘Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa BWANA umekuzukia’. Ukisoma msatri huu katika toleo la kiingereza la ESV unasema ‘Arise, shine, for your light has come, and the glory of the LORD has risen upon you’ (Isaiah 60:1). Neno ondoka ambalo kwa kiingereza ni ‘arise’ kwa fasiri ya kamusi ya kiebrania na kigiriki lina maana ya timiliza (accomplish), maliza (complete), fikia lengo (achieve) au fanikiwa (succeed). 
Kwa tafsiri hii ina maana kwamba, Mungu anayo mambo (mipango) ambayo katika mwaka 2016 anataka ufanikiwe katika kuyatimiliza na kukamilisha.

Naam na ili uweze kuyafikia yeye anaenda kukulinda kwa kufanyika ukuta wa moto utakaokuzunguka pande zote sawasawa na Zekaria 2:5 ‘Kwa maana mimi, asema BWANA, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake’.  

Zaidi katika Mitahli 8:17 imeandikwa ‘Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona’. Ni imani yangu kama:-

(i)           Ukidumu katika kumpenda Mungu kwa kuzishika amri zake

(ii)          Ukadumu katika kumtafuta

(iii)        Ukasimama vema kwenye nafasi yako kama mlinzi basi uwe na uhakika haya ambayo leo Mungu ameyafunua kwako kuhusu mwaka 2016 yatakuwa dhahiri na mwaka huu utakuwa wa baraka za pekee kuliko yote iliyotangulia. 

Mungu akubariki kwa kusoma na kuelewa maneno yake katika msisitizo huu, Biblia inasema ‘wakati wasemapo kuna amani ndipo uharibifu uwajiapo’.  Hivyo ni muhimu sana ukazingatia kumpenda Mungu na kuwa makini na maisha yako kwa kila hatua kwa mwaka huu mpya 2016. Amen!!

*************************************************************************************
Share:

USCF-SJUT NEWS

Designed by Joel Elphas @ 2015. Powered by Blogger.

Recent Posts